Wednesday, June 1, 2016

MSANII SNURA AJAZA UKUMBI WA CHUKWANI MESS CLUB

Screen Shot 2016-06-01 at 2.35.39 PM

Screen Shot 2016-06-01 at 2.35.46 PM

Screen Shot 2016-06-01 at 2.35.50 PM

Screen Shot 2016-06-01 at 2.35.55 PM

MKURUGENZI WA SMART CODES TANZANIA ATAJWA KWENYE ORODHA YA VIJANA 30 WENYE MIAKA CHINI YA 30 YA FORBES AFRICA

image
Bwana Edwin Bruno, mjasiriamali wa Kitanzania, mshindi wa tuzo ya kijana mwenye mafanikio 2015, mwanzilishi na mkurugenzi wa kampuni ya Smart Codes ametajwa katika jarida la Forbes Africa. Kila mwaka, jarida hilo hutoa orodha ya vijana 30 wenye umri chini ya miaka 30 ambao wana nafasi ya kuwa mabilionea wa baadaye.
Majina hayo yalikusanywa na kuandaliwa na mhariri wa Forbes Afrika, Ancillar Mangena ambaye naye ana chini ya miaka 30. Katika ujumbe wake, anaandika “Orodha inawakilisha vijana ambao tunaamini wana uwezo wa siku moja kuwa kwenye ukurasa wa mbele wa jarida la FORBES AFRICA, ikimaanisha watakuwa na thamani halisi ya si chini ya dola za kimarekani milioni 200, wameajiri maelfu ya watu na kusaidia kukua bara la Afrika.”
Katika mazungumzo mafupi na Edwin Bruno, anasema “Nimepewa heshima kubwa kuwa kwenye orodha hiyo, hata hivyo hii inatokana na juhudi za timu nzima pale Smart Codes. Ni wao ndio wanaofanya kazi kubwa, ambayo inaonekana ndani nan je ya nchi”
Kuhusu mafanikio yake mengine, Bruno anasema “ Ni kweli, mwaka jana programu yetu ya m-paper, ambayo inakupa nafasi ya kusoma magazeti ya Tanzania…sio vichwa vya habari, ila gazeti lote kutokea ukurasa wa kwanza hadi wa mwisho kwenye simu yako au kompyuta ilishinda tuzo ya Best Educatinal Innovation Africa, au kwa Kiswahili tuzo ya uvumbuzi bora wa kielimu barani Afrika.”
Bwana Bruno alimalizia kwa kuonesha furaha yake na kuwasihi vijana wengine kufanya kazi kwa kujituma ili waweze kufikia malengo yao au kama yale aliyosema mhariri wa Forbes Africa Ancillar, kusaidia kukua kwa bara la Afrika kiuchumi.

Kikundi cha Sanaa cha Wanafunzi wa DUCE waja na filamu ya “MAISHA YA CHUO”

DSC_4938

DSC_4924
Mmoja wa wahusika wakuu wa filamu hiyo, Bi. Rosemary Mbyalu akizungumzia namna alivyocheza uhusika katika filamu hiyo ya MAISHA YA CHUO. Katikati ni  Mwenyekiti wa kundi hilo, Bw. Kyangala Gosbert na mwisho ni Nyembo Ayubu “Mmasai wa Kigoma” ambaye pia ni msimamizi wa Habari na mawasiliano wa kundi hilo.

Kikundi cha Sanaa cha Maigizo kinachoundwa na vijana zaidi ya 30 wakiwemo wanafunzi, Walimu na wafanyakazi wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE)  kijulikanacho kama Duce Arts Group kimetambulisha rasmi filamu yao mpya ya “MAISHA YA CHUO”  ambayo wanaitarajia kuizindua Ijumaa ya Juni 3, ndani ya ukumbi wa Chuo hicho kilichopo jirani na Uwanja wa Taifa, Jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa Habari mapema leo Mei 30.2016,  Mwenyekiti wa DUCE Arts Group, Bwana Kyangala Gosbert alieleza kuwa, filamu hiyo ambayo imechezwa na wahusika wenyewe wakiwemo
 wanafunzi, wameweza kuubeba uhusika halisi wa walichokiandaa namna maisha ya Chuo yanavyokuwa na hata kupelekea matatizo kwa wanafunzi katika kufikia ndoto zao ndani ya Chuo.
“Tunawakaribisha sana siku ya  tarehe 3.6.2016, kuanzia saa 12 jioni pale ukumbi wa DUCE tutaizindua rasmi filamu hii na kiingilio ni Nakala moja ya CD ya filamu ambayo itapatikana kwa shilingi 5,000. Mlangoni. Wanafunzi wa vyuo vyote pamoja na wananchi nyoote munakaribishwa” alieleza Kyangala Gosbert.
 Filamu hiyo ya aina yake, inaelezea namna maisha ya Chuo wanayopambana nayo wanafunzi ikiwemo suala la mahusiano, ugumu wa masomo na hata kujiingiza katika masuala maovu ya ngono zembe, ulevi wa kupindukia pamoja na mambo mengine mabaya yanayopelekea kutofanya vizuri katika elimu yao ya Chuo.
Aidha katika uzinduzi huo wasanii mbalimbali wakiwemo wa Bongo Movie wanatarajia kupamba uzinduzi huo akiwemo msanii anayefanya vizuri kwa sasa Msanii Gabo.

Elephants in Tanzania reserve could be wiped out by 2022

Elephants in Tanzania

Elephants in Tanzania’s sprawling Selous Game Reserve could be wiped out within six years if poaching continues at current levels, the World Wildlife Fund warned.
Tanzania’s largest nature reserve was in the 1970s home to 110,000 elephants, but today only 15,000 remain and they are threatened by “industrial-scale poaching”.
The Selous “could see its elephant population decimated by 2022 if urgent measures are not taken,” the WWF said.
More than 30,000 African elephants are killed by poachers every year to supply an illegal trade controlled by criminal gangs that feeds demand in the Far East.
Tanzania is among the worst-affected countries with a recent census saying the country’s elephant population fell by 60 percent in the five years to 2014.
The Selous reserve is a tourist draw contributing an estimated $6 million (5 million euros) a year to Tanzania’s economy, according to a study commissioned by WWF and carried out by advisory firm Dalberg.
It is named after Frederick Selous, a British explorer, hunter and real-life inspiration for the H. Rider Haggard character Allan Quatermain in King Solomon’s Mines.
“By early 2022 we could see the last of Selous’ elephants gunned down by heavily armed and well trained criminal networks,” the report said.
The 55,000-square kilometre (21,000-square mile) reserve in southern Tanzania was named a World Heritage Site by UNESCO in 1982.
But it was put on a watch list in 2014 as poaching spiked, with six elephants killed every day and industrial activities including oil and gas exploration, as well as mining, threatening the delicate environment.
WWF Tanzania country director Amani Ngusaru said the Selous’ value, “is dependent on its large wildlife populations and pristine ecosystems.”
“Achieving zero elephant poaching is the first step to setting Selous on a path toward fulfilling its sustainable development potential,” Ngusaru said.