Watangazaji wa zamani wa kipindi cha Power Breaking kinachoruka kupitia Clouds Fm wametambulishwa kama watangazaji wapya wa Redio E FM.
Watangazaji hao walitangazwa jana katika Shindano la Shika Ndinga 2016 lililoandaliwa na E FM na kufanyika katika viwanja vya Mbagala Zakhiem jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Redio E FM, Francis Siza maarufu kama DJ Majay ndiyo aliyewatambulisha Paul James, Gerard Hando na Abel Onesmo.
![]() |
| Paul James `PJ` na Gerard Hando wakienda katika jukwaa kutambulishwa. |
![]() |
| Mkurugenzi wa Redio E FM, Francis Siza akiwatambulisha Gerard Hando na Paul James. |
![]() |
| PJ na Gerard Hando wakiwa katika picha ya pamoja na Dina Marious. |



No comments:
Post a Comment